Jumatatu, 20 Aprili 2015

FASIHI SIMULIZI; MAANA, SIFA NA TANZU ZAKE.



FASIHI SIMULIZI; MAANA, SIFA NA TANZU ZAKE.

Maana ya fasihi simulizi
 Balisidya (1983) Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwana kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake.
 Msokile, M (1992) anasema kuwa fasihi simulizi ni kazi ya sanaa inayotumia lugha ya mazungumzo ya ana kwa ana, sauti na vitendo na njia zote za mawasiliano kufikisha ujumbe kwa jamii.
 Mulokozi , M. M (1996) anasema kuwa fasihi simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi.

Sifa za fasihi simulizi
1. huwasilishwa kwa matamshi kupitia mdomo
2. ni kongwe
3. uwasilishaji wake ufungamana na vitendo
4. ni mali ya jamii na wala haimilikiwi na mtu maalumu
5. huwa na hadhira tendi (hadhira hushirikishwa)
6. hubadilika kutokana na muktadha na fanani husika
7. huwa na wakati na muktadha maalumu
8. huifadhiwa akilini mwa wanajamii husika na utendaji wake hutegemea uwezo wao wa kukumbuka

Tanzu za fasihi simulizi
Kuna tanzu kuu nne za fasihi simulizi ambazo ni semi, ushairi, maigizo na hadithi LAKINI kila tanzu ina vijitanzu vidogo vidogo kama ifuatavyo:

1. semi
·       Methali
·       Vitendawili
·       Misimu
·       Mafumbo
·       Lakabu
   
2. ushairi
·       Nyimbo
·       Ngonjera
·       Mashairi
·       Maghani

3. maigizo
·       Ngomezi
·       Vichekesho
·       Ngonjera
·       Majigambo
·       Mazungumzo
·       Malumbano ya utani
·       Mivigha
·       Ulumbi

4. hadithi
·       Hekaya
·       Visasili
·       Visakale
·       Ngano
·       Vigano
·       Soga
·       Tarihi

MAREJELEO
Tuki(2004).Kamusi ya Kiswahili Sanifu..Nairobi:  Oxford University Press East Africa Ltd

Mulokozi, M.M (1996),Utangulizi wa Fasihi Simulizi ya Kiswahili. Dares Salaam: Oxford Univeristy 
Press.      
    
Senkoro,F.E.M.K(2011) Fasihi. Dares Salaam:  KAUTTU Limited.

Msokile, M. (1992).Kunga za fasihi na lugha. Dares Salaam:  Educational Publishers and Distributors.
Wanjala, F, S, (2011), Kitovu Cha Fasihi Simulizi: Kwa Shule, Vyuo Na Ndaki, Mwanza: Serengeti bookshop.

Maoni 2 :

  1. Ukiwa umefanya kazi maisha yako yote kujenga familia na urithi, huwezi kuruhusu kivuli cha mtu wa tatu kiiharibu katika miezi michache tu. Niligundua kuwa mabadiliko ya ghafla ya tabia ya mume wangu yalikuwa kuingiliwa kiroho, si tu mgogoro wa katikati ya maisha.

    Niliwasiliana na Mystic Kakaa kwa ajili ya uingiliaji kati wa kibinafsi. Kazi yake ilikuwa ya upasuaji. Alitambua kivuli na kukiondoa kabisa bila drama yoyote ya umma. Ndani ya siku 5, umakini wa mume wangu ulirudi nyumbani kwetu na katika mustakabali wetu. Ikiwa unalinda maisha yenye thamani kubwa na unahitaji bwana anayeelewa busara, wasiliana naye kwa: dawnacuna314@gmail.com

    WhatsApp: +2349046229159

    Yeye ndiye kiwango cha dhahabu.
    Kwa uchawi wa upatanisho wa uhusiano/ndoa.

    Uchawi wa kumfanya mpenzi wako wa zamani/mwenzi wako aombe msamaha.

    Uchawi wa kumrudisha mpenzi wako/kumvutia mpenzi mpya.

    Uchawi wa kurejesha mali/pesa zilizoibiwa.

    Mabadiliko ya umbo/Uchawi wa kutoweka.

    Uchawi wa kushinda bahati nasibu/kesi ya mahakama. Na zaidi

    JibuFuta