FASIHI
SIMULIZI; MAANA, SIFA NA TANZU ZAKE.
Maana ya fasihi
simulizi
Balisidya (1983) Fasihi simulizi ni aina ya
fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwana kusambazwa kwa
wasikilizaji na watumiaji wake.
Msokile, M (1992) anasema kuwa fasihi simulizi
ni kazi ya sanaa inayotumia lugha ya mazungumzo ya ana kwa ana, sauti na
vitendo na njia zote za mawasiliano kufikisha ujumbe kwa jamii.
Mulokozi , M. M (1996) anasema kuwa fasihi
simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira
kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi.
Sifa za fasihi simulizi
1. huwasilishwa kwa
matamshi kupitia mdomo
2. ni kongwe
3. uwasilishaji wake
ufungamana na vitendo
4. ni mali ya jamii na
wala haimilikiwi na mtu maalumu
5. huwa na hadhira
tendi (hadhira hushirikishwa)
6. hubadilika kutokana
na muktadha na fanani husika
7. huwa na wakati na
muktadha maalumu
8. huifadhiwa akilini
mwa wanajamii husika na utendaji wake hutegemea uwezo wao wa kukumbuka
Tanzu za fasihi
simulizi
Kuna tanzu kuu nne za
fasihi simulizi ambazo ni semi, ushairi, maigizo na hadithi LAKINI kila tanzu
ina vijitanzu vidogo vidogo kama ifuatavyo:
1. semi
·
Methali
·
Vitendawili
·
Misimu
·
Mafumbo
·
Lakabu
2. ushairi
·
Nyimbo
·
Ngonjera
·
Mashairi
·
Maghani
3. maigizo
·
Ngomezi
·
Vichekesho
·
Ngonjera
·
Majigambo
·
Mazungumzo
·
Malumbano ya utani
·
Mivigha
·
Ulumbi
4. hadithi
·
Hekaya
·
Visasili
·
Visakale
·
Ngano
·
Vigano
·
Soga
·
Tarihi
MAREJELEO
Tuki(2004).Kamusi ya Kiswahili Sanifu..Nairobi: Oxford University Press East Africa Ltd
Mulokozi, M.M (1996),Utangulizi wa Fasihi Simulizi ya Kiswahili.
Dares Salaam: Oxford Univeristy
Press.
Senkoro,F.E.M.K(2011) Fasihi. Dares Salaam: KAUTTU Limited.
Msokile, M. (1992).Kunga za fasihi na lugha. Dares Salaam: Educational Publishers and Distributors.
Wanjala, F, S, (2011), Kitovu Cha Fasihi Simulizi: Kwa Shule, Vyuo
Na Ndaki, Mwanza: Serengeti bookshop.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni