Jumatatu, 20 Aprili 2015

FASIHI SIMULIZI; MAANA, SIFA NA TANZU ZAKE.



FASIHI SIMULIZI; MAANA, SIFA NA TANZU ZAKE.

Maana ya fasihi simulizi
 Balisidya (1983) Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwana kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake.
 Msokile, M (1992) anasema kuwa fasihi simulizi ni kazi ya sanaa inayotumia lugha ya mazungumzo ya ana kwa ana, sauti na vitendo na njia zote za mawasiliano kufikisha ujumbe kwa jamii.
 Mulokozi , M. M (1996) anasema kuwa fasihi simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi.

Sifa za fasihi simulizi
1. huwasilishwa kwa matamshi kupitia mdomo
2. ni kongwe
3. uwasilishaji wake ufungamana na vitendo
4. ni mali ya jamii na wala haimilikiwi na mtu maalumu
5. huwa na hadhira tendi (hadhira hushirikishwa)
6. hubadilika kutokana na muktadha na fanani husika
7. huwa na wakati na muktadha maalumu
8. huifadhiwa akilini mwa wanajamii husika na utendaji wake hutegemea uwezo wao wa kukumbuka

Tanzu za fasihi simulizi
Kuna tanzu kuu nne za fasihi simulizi ambazo ni semi, ushairi, maigizo na hadithi LAKINI kila tanzu ina vijitanzu vidogo vidogo kama ifuatavyo:

1. semi
·       Methali
·       Vitendawili
·       Misimu
·       Mafumbo
·       Lakabu
   
2. ushairi
·       Nyimbo
·       Ngonjera
·       Mashairi
·       Maghani

3. maigizo
·       Ngomezi
·       Vichekesho
·       Ngonjera
·       Majigambo
·       Mazungumzo
·       Malumbano ya utani
·       Mivigha
·       Ulumbi

4. hadithi
·       Hekaya
·       Visasili
·       Visakale
·       Ngano
·       Vigano
·       Soga
·       Tarihi

MAREJELEO
Tuki(2004).Kamusi ya Kiswahili Sanifu..Nairobi:  Oxford University Press East Africa Ltd

Mulokozi, M.M (1996),Utangulizi wa Fasihi Simulizi ya Kiswahili. Dares Salaam: Oxford Univeristy 
Press.      
    
Senkoro,F.E.M.K(2011) Fasihi. Dares Salaam:  KAUTTU Limited.

Msokile, M. (1992).Kunga za fasihi na lugha. Dares Salaam:  Educational Publishers and Distributors.
Wanjala, F, S, (2011), Kitovu Cha Fasihi Simulizi: Kwa Shule, Vyuo Na Ndaki, Mwanza: Serengeti bookshop.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni