Jumanne, 17 Machi 2015

NADHARIA YA VIKOA VYA MAANA NA UHIPONIMIA

NADHARIA YA VIKOA VYA MAANA NA UHIPONIMIA
Maana ya nadharia
Mdee  (2011) nadharia ni mpango wa mawazo uliotungwa ili kueleza jinsi ya kufanya au kuelekeza jambo fulani.
Sengo (2009) nadharia ni wazo kuu, fikra kuu, mwongozo mkuu wa mtu, watu,  au jamii ya ya pahala fulani, wakati fulani na kwa sababu fulani.

Nadharia ya vikoa vya maana
Dirk (2010) anasema kuwa vikoa vya maana ni jozi za maneno yenye maana zinazohusiana  ambazo maana zake zinategemeana na kwa pamoja zinatoa dhana ya kimuundo yenye uhalisia ndani yake.
Kwa mujibu wa Wikipedia, kikoa cha maana ni msamiati wa kiufundi katika taaluma ya isimu ambao unaeleza kikundi cha maneno yanayohusiana kimaana.

 Nadharia ya uhiponimia
Briton (2000) anaeleza kuwa uhiponimia ni uhusiano wa kiwima ambapo hujumuishwa katika fahiwa na neno jingine. Kwa mfano fahiwa ya mgomba, mahindi na maharage zimejumuishwa katika mimea.
Matinde (2012) hiponimu ni neno ambalo lina maana mahususi amabayo hujumuishwa katika maana ya neno ambalo lina maana pana na uhiponimia ni uhusiano wa kifahiwa uliopo baina ya neno lenye maana mahususi na neno linguine lenye maana jumuishi.

 Kwa mantiki hii tunabaini kuwa Tofauti kuu kati ya nadharia ya vikoa vya maana  na uhiponimia ni kwamba vikoa vya maana hujumuisha maneno yenye maana jumuishi wakati uhiponimia huwa na maneno yenye maana mahususi. Kwa mfano neno mnyama ni kikoa cha maana ambacho hujuisha simba, nyani, chui, nguruwe, pundamilia, tembo na kadhalika wakati neno pundamilia ni hiponimu amabayo huwa na maana mahususi yaani mnyama mwenye mistari mweupe na myeusi katika ngozi yake

                                       


                                    MAREJELEO
                                     
Briton L.J. (2000). The structure of modern English. A linguistic Introillustrated Edition. John Benjamin Publishing Company.

Dirk G,(2010). Theories of Lexical Semantics. Oxford University Press: New York

Mdee, J, S (2010) Nadharia na historia ya leksikografia. TUKI: Dares salaam.

Matinde, R.S.(2012). Dafina ya Lugha Isimu na Nadharia, Kwa Sekondari, vyuo vya kati na            vyuo vikuu, Serengeti Education Publishers(T) Ltd: Mwanza.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni